A. Muingiliano kati ya Sintaksia na Mofolojia (Mofo-Sintaksia)
Rubanza
(1996) anasema, mofolojia ni taaluma inayoshughulikia vipashio vya lugha katika
kuunda maneno.
(Rubanza,
1996) anatupatia muingiliano wa sintaksia na mofolojia kama ifuatavyo:-
kipashio
cha msingi katika uchambuzi wa kimofolojia ni neno ambalo, ambalo pia hutumika
kuunda darajia ya sintaksia. Pia maumbo ya kimofolojia huathiri vipengele vingine
vya kisintaksia
Mfano: (
i ) M-toto a-napika (umoja)
(ii ) Wa-toto wa-napika (wingi)
Katika
mifano hii, tunaona kwamba mofimu //m// na //wa// katika upande wa kiima zimeathiri
utokeaji wa “a”- na “wa” katika upande wa kiarifu.
Pia
kanuni za mfuatano wa mpangilio wa mofimu au viambishi zikifuatwa huunda maneno
katika miundo ya kisintaksia.
Mfano:
Alioga → A –
li – og – a
Analiona → A- na – lim- a
Hivyo
kipengele cha umoja na uwingi katika maumbo ya kimofolojia ndicho kinacho
athiri umbo linalofuata jina na kuathiri muundo wa sentensi nzima
Mfano:
Mganga anaandika barua
Waganga
wanaandika barua
Matinde
(2012) na Habwe & Karanja (2004)
katika maelezo yao wanatupatia muingiliano uliopo baina ya sintaksia na
mofolojia kama ifuatavyo:-
1.
Mofolojia ndio inayotupatia kizio kidogo kabisa cha kisintaksia, hii ina maana
kuwa, kuna baadhi ya dhana ambazo hutumika katika matawi yote mawili ya
kisarufi yaani mofolojia na sintaksia, mfano “neno”, hiki ni kizio cha juu
kabisa cha mofolojia lakini pia neno ndicho kizio kidogo kabisa cha sintaksia.
2.
mofimu huru ndizo huungana na kutupatia viwango mbalimbali vya kisintaksia kama
vile kirai, kishazi, tungo na hata sentensi.
Mfano: //Baba// + //yetu// →
Baba yetu (kirai)
//Gari// + //zuri// → Gari
zuri (kirai)
//Juma// + //Cheza// + //mpira// → Juma cheza
mpira (sentensi)
3.
Sintaksia na mofolojia huingiliana kupitia dhana ya urejeshi, ambapo kunakuwa
na viambishi (Mofolojia) hurejea umbo lingine katika sentensi (sintaksia) na
kufanya pawe na uhusiano baina ya maumbo hayo.












Hapa
tunaona maumbo ya urejeshi ya “ye” na “lo” yanarejerea mtenda. Kwa upando mwingine
umbo la “ji” linarejerea kifaa kilichotumika katika tukio. Kwa ujumla maumbo ya
urejeshi ndio yanayolazimisha kutokea kwa maumbo mengine katika sentensi au
tungo ili kukamilisha dhana inayozungumziwa.
4.
Kuna baadhi ya maumbo (mofolojia) hayawezi kuwa na maana yoyote endapo kama
yatasimama peke yake, lakini maumbo hayo hayo
yakiambatanishwa na maneno mengine katika sentensi huweza kupata maana.
Maumbo hayo ni kama vile vihusishi “ya”, “la”, “ya”, “na”, “ni”, “kwa” na “kama”.
Mfano: Gari la juma (“la” lina maana ya
umilikishi).
Mutachuba na wadugu wanaimba (“na” –
kiunganishi).
Mzilani
atasafiri kesho kama atapata ruhusa (“kama” ina maana ya uwezekano).
Asha anatembea kwa miguu (“kwa” – namna
tendo linavyofanyika).
Juma ni mwizi (“ni” inathibitisha
kuwepo kwa tabia).
Kompyuta ya baba (“ya”- kimilikishi).
5. Kuna baadhi ya maumbo (mofolojia) huweza
kubadili sentensi (sintaksia) kutoka hali moja na kwenda hali nyingine.
Mfano: 1 (a)
Huyu ni mwizi (ni- hali yakinifu)
(b) Huyu si mwizi (si – hali kanushi)
2. (a) Mtoto anaimba (na - hali iliyopo)
(b)Mtoto
ameimba (me – hali timilifu)
3 (a)Juma
aliimba akapewa zawadi
(b)Juma
angeimba angepewa zawadi (“nge”
imebadili kabisa mauombo katika
sentensi hii)
6.
Dhana ya uelekezi; sintaksia na mofolojia huingiliana kupitia uelekezi.
Uelekezi ni hali ya kitenzi kuruhusu au kutoruhusu nomino kufuata mbele yake (Matinde,
2012). kuna baadhi ya maumbo (mofolojia) hususani vinyambuzi vinapowekwa katika
kitenzi, huweza kuamua kuwa ni idadi za nomino kufuata ama kutofuata kabisa.
Mfano:
( i ) Dada amempik- i- a baba chakula (nomino
mbili).
Hapa tunaona umbo (kinyambuzi) “ i ”
kimeruhusu nomino mbili kufuata baada ya kitenzi.
( ii ) Baba amempig – a mwizi
Hapa pia tunaona kinyambuzi “a” kimeruhusu
nomino moja kufuata.
7.
Kiambishi ngeli (mofolojia) huweza kuathiri utokeaji wa maumbo ngeli mengine
katika sentensi (sintaksia). Hii ina maana kuwa maumbo ngeli (mofolojia) kwa kiasi
kikubwa hutawala maumbo mengine katika sentensi (sintaksia)
Mfano:
(i) M-toto a-nacheza (“m”-umbo ngeli lenye kubeba dhana ya umoja ndilo
lililopelekea kutokea kwa “a” katika kitenzi anacheza
(ii) Wa-toto wa-nacheza (“wa”-
ni umbo ngeli 2, lenye kubeba dhana ya wingi na ndilo lililopelekea utokeaji wa umbo
“wa” katika kitenzi wanacheza.
(iii) Mwalimu alikuwa anafundisha
(iv) Walimu walikuwa wanafundisha
Tunaona
katika mifano hii maumbo ya umoja na uwingi wa maneno mwalimu na walimu
yameathiri mpangilio mzima wa sentensi
Maumbo ngeli (mofolojia) kwa kiasi kikubwa ndiyo
yanayoleta upatanisho wa kisarufi katika sentensi (kisintaksia).
8.
Kuna mabadiliko ya kimofosintaksia ambayo hutokea kwa kuhusisha dhana zote
mbili za sintaksia na mofolojia. Kwa kiasi kikubwa mabadiliko haya hutokea ili
kuleta upatanisho wa kisarufi katika tungo. Neno moja katika sentensi linaweza
pelekea mabadiliko katika neno lingine linalofuata.


Wake


(ii) Miaka iake → Miaka i a ke
Yake


Mtoto mdogo
Katika
mifano hapo juu, tunaona mabadiliko mbalimbali yametoke. Katika mfano (i)
tunaona neno “mtoto” limepelekea badiliko la uyeyushaji wa irabu “u” na kuwa
“w” na kupata neno “wake” badala ya “uake”. Katika mfano (ii) pia tunaona
badiliko la irabu “ i” kuwa “y” kutokana na uyeyushaji, hivyo tunapata neno “yake”
baada ya “iake”. Lakini pia katika mfano (iii) tunaona badiliko la kupunguzwa
kwa “u” kati ya “m” na “d”, badiliko hili linatokana na udondoshaji uliofanyika
ili kuleta urahisi katika kukitamka kirai “mtoto mdogo”
Habwe
na karanja (2004) katika maelezo yao, wanaongeza baadhi ya muingiliano kati ya
mofolojia na sintaksia kama ifuatavyo:-
9.
Sintaksia na mofolojia huingiliana katika utendaji; kuwa vyote hujihusisha na
kuchunguza mpangilio katika Lugha. Mofolojia huchunguza mpangilio wa mofu
katika neon, wakati sintaksia huchunguza mpangilio wa maneno katika sentensi.
10
sintaksia na mofolojia kwa pamoja huhusisha au hutumia taratibu (hatua) za
kisayansi katika uchunguzi wa lugha ya binadamu.
11.
Sintaksia na mofolojia kwa pamoja
huchunguza muundo wa ndani na muundo wa nje wa lugha. Mofolojia kwa upande wake
huchunguza muundo wa ndani na muundo wanje wa maneno katika lugha (Matinde,
2012).
Mfano.
Neno
|
Muundo
wa ndani
|
Muundo
wa nje
|
Mutu
|
Mutu
|
Mtu
|
Mbwa
|
Mmbwa
|
Mbwa
|
Nje
|
Nnje
|
Nje
|
Katika
upande mwingine sintaksia huchunguza muundo wa ndani na muundo wa nje wa
sentensi (sintaksia)
Mfano: (i) Juma cheza mpira (muundo wa ndani)
Juma
anacheza (muundo wan je)
(ii) Asha anacheza vizuri mpira wake (muundo
wan je)
Asha
anacheza mpira wake vizuri (muundo wa ndani)
12.
Kwa baadhi ya dhana kama vile virejeshi (mofolojia) zikitumika katika sentensi
huweza kuibadili sentensi sahili na kuwa sentensi tegemezi (kishazi tegemezi)
Mfano: (a) Mtoto anasoma kitabu (sentensi sahili)
Mtoto anayesoma
kitabu (kishazi tegemezi)
(b)
kiti kimevunjika (sentensi sahili)
Kiti kilichovunjika
(kishazi tegemezi)
(c), kuku
amenunuliwa (sentensi sahili)
Kuku aliyenunuliwa
(kishazi tegemezi)
B. Muingiliano kati ya Sintaksia na Fonolojia (Mofo-Fonolojia)
1.Uhusiano
baina ya fonolojia na sintaksia, Massamba na wenzake (wameshatajwa) wanafasili
fonolojia kuwa ni uchambuzi wa mfumo wa sauti katika lugha zinavyoungana ili
kujenga maneno yanayokubalika katika lugha kwa hiyo tunaweza kusema kuwa
kuungana kwa vitamkwa ili kujenga maneno yanayokubalika katika lugha fulani hutegemea
mpangilio sahihi wa vitamkwa. Na kwa kuwa neno ni kiwango cha msingi cha
uchambuzi katika sintaksia, basi fonolojia inauhusiano wa moja kwa moja na
sintaksia.
Mifano
ifuatayo huthibitisha hoja hii
(I)
“Anapika” hii ni neno lakini pia ni
sentensi hivyo huweza kuchanganuliwa kifonolojia kama ifuatavyo a/n/a/p/i/k/a/, mpangilio wa sauti umeunda
neno “anapika”.
(II)
(a)
baba limeundwa na ( limeundwa kwa muundo wa silabi wa KIKI)
(b) Abab
limeundwa na ( limeundwa kwa IKIK)
Katika
mfano 2a tunaona neno “baba” lina maana na limefuata kanuni na mpangilio
unaokubalika wakati mfano 2b neno abab halina maana katika lugha ya Kiswahili
kwa sababu halina mpangilio mzuri wa fonimu. Kwa mifano hii tunaona kwamba,
hatuwezi kuwa na miundo mikubwa katika sentensi bila kuwa na mpangilio sahihi
wa sauti katika lugha. kwa hiyo sintaksia haiwezi kukamilika bila fonolojia.
2.
Fonolojia pia ndiyo chimbuko la sentensi kwani, sauti (konsonanti na irabu)
ndizo huungana na kutupatia neno (maneno) ambayo ndiyo huungana kutupatia
kirai, kishazi na hata sentensi ambavyo hivi vyote ni viwango vya kisintaksia (Nchimbi,
2008)
3. Pia
kanuni za mfuatano na mpangilio wa mofimu au viambishi zikifuatwa huunda maneno
katika miundo ya kisintaksia mfano.
(i)
Alicheza = a-li-chez-a
(ii)
Anaimba
= a- na- imb-a
Kama unahitaji huduma ya kuandikiwa makala katika tovuti yako, au huduma yoyote basi wasiliana nami kupitia:-
SIMU: +255 755 987 604, +255 789 198 345
E-MAIL: reubentanzania@gmail.com
Massamba
D.PB na wenzake (1999) Sarufi miundo ya
Kiswahili sanifu: Sekondari na vyuo.
Dar es salaam.TUKI.
Rubanza
Y.I (1996) Mofolojia ya Kiswahili:
Dar es salaam: Chuo kikuu huria cha Tanzania.
TUKI (2004) Kamusi ya Kiswahili
sarufi: Dar es Salaam.TUKI.
Nchimbi A. S (2008) OFC, Kiswahili: Dar es Salaam. Chuo kikuu Huria cha Tanzania.
Habwe
J. & Karanja P.C (2004) Misingi ya
sarufi ya Kiswahili:Nairobi. Phoenix Publishers Ltd.
Matinde
R.S (2012) Dafina ya lugha Isimu na
Nadharia kwa Sekondari, Vyuo vya kati na vyuo vikuu :Mwanza. Serengeti
education publishers (T) Ltd.
Massamba,D.P.B
na Wenzake (2004) Fonolojia ya Kiswahili (FOKISA), Sekondari na Vyuo:
Dar es salaam
Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI).
Jamani! kwanini somo la Kiswahili huonekana kama gumu sana kwa baadhi ya wanafunzi wa upili hasa kwa kidato cha 5 an 6?
JibuFutawao hupendelea sana lugha ya kigeni...na kutopenda kiswahili
FutaHii Ni kwa sababu baadhi ya wanafunzi wao wameathiriwa na lugha ya kwanza kabisa.Hii ndiyo sababu huenda wakaiona somo La kiswahili kuwa mgumu
JibuFutaMaoni haya yameondolewa na mwandishi.
JibuFutaUsitume free domain kama. Blogspot.com na za wordpWord.com tengeneza yako mwenyewe upige hella. Ntafte nkuelekeze
JibuFutatupia namba yako nikuchek
Futabeast, tupia namba yako nikuchek
JibuFutasamahan ndugu yangu kwa kuchelewa kujibu ujumbe wako! namba yangu ni 0755987604
FutaIpo vizur
JibuFutasafi sana, naandaa nyuzi nyingine!
JibuFutaNaomba namba yako
JibuFuta0755 987 604
FutaNingependa kutambua uhusiano Kati ya fonolojia na mofolojia
JibuFutaUsijal ndg, muda si mrefu ntachapisha makala juu ya uhusiano wa Fonolojia na Mofolojia
FutaNaomba kufahamu kuhusu michakato na kanuni za kimofo-fonolojia/kimofo-fonemiki!
JibuFutaKuna sina ngap za maneno? Tuma wataalam watano
JibuFutaAhsnte
JibuFutaNaomba unipatie ufanano wa fonetiki na fonoloji angalau pointi tano(5)
JibuFutaNaomba uhusiano kati ya fonolojia na sintaksi.hoja (5)
JibuFutaNitmie hyo makala kiongozi
JibuFutaMakala nzuri naomba kutumiwa kikashani
JibuFutaKwa kutolea ithibati ya kiisimu, ningependa unisaidie na uhusiano uliopo baina ya fonolojia na mofolojia
JibuFuta