Jumatano, 28 Novemba 2018

MJASIRIAMALI--TOP 10 ZA KUKUPA MTAJI KWA HARAKA


#1: Taaluma uliyonayo (elimu)

Unaweza kupata mtaji kwa kuitumia vyema elimu yako! Kuna mambo mawili ya kufanya ili upate mtaji katika njia hii. Mosi, ni kujiajiri mwenyewe kupitia taaluma uliyonayo.
Mfano.
1.       kama wewe ni muhandisi wa umeme, basi unaweza ukaanzisha huduma ya kuweka umeme majumbani (domestic electirical installation). Kupitia hii huduma, unaweza kupata mtaji na kisha ukafungua duka la vifaa vya umeme. Ni watu wengi waliofanikiwa kupata mitaji mikubwa kwa kupitia njia hii! Nina mfano wa technician mmoja wa kiwanda cha saruji kilichopo Songwe- Tanzania (Zephania Lulyeho), yeye alianza kufanya hivyo kama anajaribu, lakini sasa hivi anamiliki kampuni yake ya JAZA yenye kujishughulisha na masuala ya kufanya electrical installation.
2.       kama wewe ni daktari, basi unaweza kuanzisha kituo kidogo cha afya! Hata kama kiwe na uwezo wa kutoa huduma ya kwanza, au kutoa vipimo hata viwili (mf, malaria na taifodi) kinatosha kuanzia. Baada ya kupata mtaji mzuri, basi utaweza kufungua duka la madawa! Kwani utakuwa tayari una cheti cha afya, lakini pia utakuwa na kibari cha kukuruhusu kuuza madawa na vyakula, mfano cheti cha TFDA kwa upande wa Tanzania.
3.       kama wewe ni mwalimu, basi unaweza ukaanzisha kituo cha masomo kwa muda wa ziada (tution). Kituo hiki utakipatia majukumu kadha wa kadha kama vile, kozi fupi ya lugha ya Kiingereza, kuwanoa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari na Kuwanoa wale wanaohitaji kurudia kufanya mitihani ya kidato cha 4 & 6. Haya majukumu ni vigumu kufanywa na mtu mmoja kwa ufanisi, hivyo unashauriwa kuungana na watu wenye nia na wenye vigezo vya kufanya kazi hiyo, hata kama iwe nikwakugawana faida.
Lakini, pili (2) ni kuajiriwa katika taasisi, serikali ama mtu binafsi

#2: Kuomba mtaji kwa wanafamilia, ndugu na jamaa

 Hapa pia kuna mambo ya kuzingatia ili upate mjati kwa ndugu au jamaako wa karibu
v  Onyesha uwajibikaji
v  Msaidie kazi kwa uaminifu wote
v  Tambua nini anapendelea huyo ndugu yako  
v  Mpe mawazo na mbinu za kuiendeleza biashara yake
v  Utakapofikia wakati wa kumwomba mtaji, omba mtaji kidogo
v  Baada ya kupewa mtaji, hakikisha unamshirikisha katika biashara yako. Hii ni pamoja na kumpatia taarifa juu ya maendeleo ya biashara yako.

#3: Fani/ kipaji

Unaweza kupata mtaji kupitia kipaji chako! Lakini pia unaweza kukifanya kipaji chako kama ndiyo ajira yako. Ili kukifanya kipaji kuwa ajira, unashauriwa pia kupata mawazo mapya kutoka kwa watu, wateja, au washabiki wako, lakini pia soma vitabu mbali mbali vinavyohusiana na kipaji chako. Mawazo haya ndiyo yatakayokufanya uwe mbunifu katika fani yako. Unapofanya kazi kupitia kipaji chako, ni vyema pia ukazingatia uhusiano wa kazi zako na soko la kimataifa. Katika makala zijazo, tutajadili zaidi juu ya jinsi ya kutafuta masoko ya kimataifa kwa lazima. Mfano, msusi, mfinyanzi, mchoraji, mchongaji, mwana muziki, mwandishi nk, hawa wote wanawezaje kupata soko la kimataifa kwa lazima. Maana, inatakiwa umlazimishe mtu kuwa mteja wako pasipo yeye kujua kama unamlazimisha kuwa mteja wa bidhaa yako.

#4: Uzoefu katika kufanya kitu fulani

Katika upande wa masuala ya ajira imekwisha zoeleka kwamba, ili upate ajira basi unatakiwa uwe na uzoefu wa miaka kadhaa kazini katika kitengo unachoomba kazi. Ukweli ni kwamba katika mfumo wa uchumi na biashara kwa sasa, mwajiri anaajiri mtu ambaye anaweza kumrahisishia kazi bila kufundishwa pindi anapokuwa akitumikia nafasi yake ya kazi ili kuepusha hasara na gharama ambazo hazikuwa za lazima. Lakini pia, hauwezi kupata uzoefu bila kuanza. Hii nina maana kwamba, ili upate uzoefu basi fanya kazi hata kwa mfumo wa kujitolea, kwani kupitia kujitolea utaweza kujuana na watu wengi zaidi na zaidi, na hicho ndicho mshahara wako.

#5: Ujuzi

Ujuzi nao ni moja ya mambo muhimu sana katika kukurahisishia kupata mtaji. Hapa zaidi kinachotiliwa maanani ni ufundi ambao mtu anaupata hata pasipokuwa na elimu kubwa. Kupitia ujuzi, unaweza kuwa fundi ujenzi wa kisasa, fundi wa vifaa vya kielekitroniki kama vile, redio,TV,kompyuta,pasi za umeme n.k. watu wengi sana wana ujuzi mbalimbali, lakini hawana nidhamu ya pesa. Kutokuwa na nidhamu ya pesa, kunawafanya wawe na maisha yale yale kila mwaka, na hatimaye kuuona ujuzi wao kama hauwasaidii kabisa katika maisha yao! Jamani TUBADILIKE KATIKA JINSI YA KUFIKIRI MAMBO

#6: Fanya Kitu unachokipenda

Kufanya kitu unachokipenda ni njia mojawapo muhimu ya kukuongezea mtaji. Kuna watu wana mitaji midogo na wameshindwa kuiendeleza mitaji hiyo kutokana na kufanya kitu/biashara wasioipenda. Ni ukweli kuwa, kuna baadhi ya watu hufanya mambo, kazi au biashara kwa kufuata mihemko ya wazazi, ndugu au rafiki zao, lakini ndani ya moyo mioyo yao hawaridhiki kabisa. Hali hii itakufanya upunguze ukaribu na kile unachokifanya, lakini pia unaweza kukosa ubunifu wa kazi/ biashara hiyo kutokana na kutoipenda.

#7: Omba mkopo

Kama una nia kweli ya kufanya biashara, na una vigezo vya kuzifanya taasisi za kifedha kukuamini, bai omba mkopo.
ANGALIZO: 1
Usiombe mkopo wa kibiashara, endapo kama haujaanza biashara, maana fedha ya mkopo siyo fedha ya kuanzisha biashara, bali ni fedha ya kuendeleza biashara. Nimeeleza mambo mengi sana katika kitabu change kinachohusu masuala ya mikopo, na siku siyo nyingi nitakichapisha ili nawe msomaji wangu ujifunze mengi juu ya masuala ya mikopo kutokana na mengi niliyojifunza kuhusu mikopo.

ANGALIZO: 2
Usichukue mkopo endapo kama haujafanya utafiti wa kutosha juu ya biashara unayoifanya/unayotaka kuifanya.

#8: Uuzaji wa rasilimali

Hii nayo ni njia ya kupata mtaji lakini sikushauri sana kuitumia kwani, siyo rahisi kuirudisha rasilimali ambayo umekwishaiuza. Kama mtu unayeanza kupambana ili upate msingi mzuri wa maisha, si vyema kuwa na tabia ya kuuza vitu. Hii ni kutokana na ukweli kuwa, bei utakayouzia kwa kiasi kikubwa siyo bei rafiki. Lakini kama ukikwama sana na ukaona njia zingine huwezi kuzitumia basi unaweza ukauza, lakini uwe na uhakika wa kuirusha rasilimali hiyo unayoiuza.

#9: Kushirikiana na watumishi wa serikali

Kuna baadhi ya watumishi wa serikali hawana muda wa kuzalisha mishahara yao. Lakini wapo wengine ambao hata hawana elimu ya fedha. Kutokana na pengo hili, kama mjasiliamali usiye na mtaji, unatakiwa kupanga biashara na mwelekeo wa hiyo biashara, na kisha ukamshirikisha mtumishi ambaye anaonekana kutokuwa na uwekezaji wowote wa fedha yake.
ANGALIZO
Mjasiriamali unatakiwa kuwa na tarifa za uhakika juu ya biashara unayoipendekeza, na hizi taarifa unaweza kuzipata kupitia kufanya utafiti wa kutosha juu ya biashara hiyo. Mfano, je ni biashara ya msimu?, faida yake, hasara zake zinasababishwaje? Jinsi ya kuzuia hasara, wateja wa biashara hiyo ni watu gani? N.k. kwa kufanya hivyo, utaweza kufanya biashara ambayo itakunufaisha wewe pamoja na Yule aliyewekeza fedha yake katika biashara hiyo.

#10: Ufugaji

Kama una mtaji wa eneo, basi fanya ufugaji wa mifugo ili upate mtaji unaouhitaji ndani ya kipindi kifupi. Kuna mifugo wengi ambao unaweza ukawafuga, mfano, kuku wa kienyeji, bata wa kawaida, bata maji, bata mzinga, sungura, kanga, kwale, nguruwe n.k. hawa wote wana uwezo wa kukupatia mtaji kwa muda mfupi. Cha muhimu ni kufugakibiashara, na kutafuta masoko yenye tija.
Katika biashara, mambo ya muhimu unayotakiwa kuwanayo ni UKWELI na UAMINIFU! Utapata wateja waminifu na utapata mtaji hata bila kuomwomba mtu, ila yeye atakuletea fedha yake uifanyie uzalishaji

Nakushukuru kwa kufuatilia makala zangu katika blog yangu na katika kurasa zangu za mitandao ya kijamii. Usikose kufuatilia makala zangu zingine, ni rahisi sana, ingia kwenye blog yangu kisha bofya kitufe  follow by e-mail. Mpaka hapo utakuwa umefanikiwa kupata makala zangu mpya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MUINGILIANO KATI YA SEMANTIKI NA PRAGMATIKI---ACADEMICIAN BLOG

UTANGULIZI Maana ya Semantiki Richmond (2012   anafafanua maana ya Semantiki kwamba ni tawi la isimu ya lugha linalohusu viyambo ...