Ijumaa, 9 Februari 2018

UNYAMBULISHAJI - Nduni za Unyambulishaji



CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ASKOFU MKUU YAKOBO

KITIVO CHA SANAA NA SAYANSI ZA JAMII
IDARA YA LUGHA, ISIMU NA FASIHI

JINA LA KOZI                                           : MOFOLOJIA YA KISWAHILI
MSIMBO WA KOZI                                  : SW 232
JINA LA MHADHIRI                                : SOTE, A
AINA YA KAZI                                          : KAZI YA KIKUNDI YA SEMINA
KUNDI                                                         :Na. 08


MAJINA.

Na

                   JINA

  NAMBA YA USAJILI

   SAHIHI
01
BUYA  FADHILI, A
BAED2  45283

02
KINUNDA  JOSEPH
BAED2  45332

03
KITIKITI  MARIAM
BAED2  45334

04
KOMBA  ADELHEMA
BAED2  45337

05
MBUNDA  CLEMENCE, L
BAED2  45360

06
MTEGA THEOBIAS, T
BAED2  45383

07
MYOMBE  BARAKA
BAED2  45402

08
REUBEN  JOHN,K
BAED2 45431

09
NGIMBA  SHAADA
BAED2  45469



SWALI:      JADILI KWA HOJA NA MIFANO NDUNI ZA UNYAMBULISHAJI.

UTANGULIZI
Kwa ujumla kazi hii ina sehemu kuu tatu, ambazo ni Utangulizi, Kiini cha kazi na Hitimisho. Utangulizi una husisha maana ya Unyambulishaji kutokana na mawazo ya wataalamu mbalimbali na Maana ya Wanakikundi juu ya Unyambulishaji. Sehemu ya pili inahusu Kiini cha kazi hii, ambapo Nduni zipatazo tisa zimeweza kujadiliwa zikiwa na mifano yake, na Sehemu ya tatu ni hitimisho, ambalo limebeba maoni kuhusu jinsi ya kutofautisha dhana ya Unyambulishaji na Uambishaji (Uambatizi).

Maana ya Unyambulishaji kwa mujibu wa mawazo ya Wataalamu mbalimbali.

BAKIZA (2010) wanasema kuwa Unyambulishaji ni muendelezo wa shina la neno kwa kuongezea viambishi ili kujenga neno jipya.

Kihore (2009) naye anasema kuwa,  unyambulishaji ni tendo la kupachika vipashio kwenye kiini ili kujenga (ma) neno.

Unyambulishaji ni utaratibu wa kupachika viambishi kwenye mzizi ili kuunda maneno mapya (Massamba, 2004).

Hivyo basi, Unyambulishaji ni tendo la kuongeza viambishi katika mzizi wa neno yaani kabla ya mzizi au baada ya mzizi wa neno, ambapo matokeo yake yaweza kuwa ni kubadili maana ya neno, kategoria ya neno au yawezakuwa kubadili aina ya neno ndani ya kategoria moja ya neno.




NDUNI  ZA  UNYAMBULISHAJI

TUKI (2013) Wanatupatia maana ya neno “Nduni” kuwa, ni “sifa maalumu ya kitu”. Kwa maana hiyo basi, Nduni za Unyambulishaji ni sifa za unyambulishaji, na zifuatazo ni nduni za Unyambulishaji kwa mujibu wa Nchimbi (2008).

1.      Unyambulishaji unatokea au unafanyika katika kategoria za maneno  au katika maneno yanayokubali kubadili umbo lake. Hii ikiwa na maana kuwa, maneno yanayokubali kupokea mofu mbalimbali katika umbo lake .
Mfano.
Mtoto > ki-toto, Tu-toto
Bakuli > ki-bakuli, vi-bakuli
Taifa > M-taifa, U- taifa, ki-taifa.
Kwa upande mwingine unyambuzi hauwezi kutokea au kufanyika katika maneno yasiyokubali kubadili umbo lake.
Mfano.
Viunganishi : na, kwa, katika, au, pia
Vihisishi : Mfano, loo !, ewe !, la hasha !
Vihusishi : Mfano, la, ya, cha, kwa
Vielezi asilia : Mfano, mapema, asubuhi, sana
2.      Maneno yanayoundwa kutokana na unyambulishaji yanaweza kupewa maana ama mpya au maana ya ziada. Kwa mantiki hii, kumbe unyambulishaji unaweza kubadili maana ya neno, kwa kutoa matokeo ya maana mpya ya neno.
Mfano.
Chumba > Chumba-ni
Pig-a > Pig-o
Taifa > U-taifa
Kasuku > U-kasuku
Jiko > U-jiko
3.      Unyambulishaji unaweza kubadili kategoria ya neno, kutoka katika kategoria moja na kwenda katika kategoria nyingine ya neno.
Mfano.

Kutoka kategoria ya Kitenzi kwenda kategoria ya Nomino.
Pig-a > Pig-o, Pig-an-o
Tuli-a > M-tulivu
Karibisha > M-karibishaji
Sawazisha  > Sawaz-ish-o


Kutoka kategoria ya Kielezi kwenda kategoria ya Kitenzi
Mfano.
Rahisi > Rahis-ish-a
Karibu > Karib-i-a, Karib-ish-a
Sawa  > Sawaz-ish-a

Kutoka kategoria ya Nomino kwenda kategoria ya Kielezi

Mfano.
Katiri > Ki-katiri
Chumba > Chumba-ni
Mzalendo > Ki-zalendo
Afande > Ki-afande.


Kutoka kategoria ya Kivumishi kwenda kategoria ya Kitenzi

Mfano.
Fupi > Fupisha
Nene > Nenepesha
Bora > Boresha.

4.      Unyambulishaji pia unauwezo wa kubadili aina ya neno katika kategoria moja . Hii ina maana kuwa ndani ya kategoria moja ya neno, Neno linaweza kubadilishwa aina kutoka aina moja ya neno na kwenda aina nyingine ya neno pasipo kuathiri au kubadili kategoria ya neno husika. Kwa mfano, Katika kategoria ya Nomino, Neno linaweza kubadilishwa kutoka katika aina ya nomino za kawaida na kuwa nomino dhahania.
Mfano.
Chumba > U- chumba
Jiko > U-jiko
Mzee > U-zee
Jambazi > U-jambazi
Kenge > U-kenge.

5.      Unyambulishaji una uwezo wa kuonyesha kauli katika kitenzi husika, na kumfanya mtumia lugha atambue kuwa ni dhana gani inayozungumziwa au inayofanyika katika kitenzi. Hivyo kupitia mnyambuliko tunaweza kupata kauli zifuatazo:-
Kauli ya kutenda:         Mfano, Pig-a, Som-a, Imb-a.
Kauli ya Kutendwa:    Mfano, Pig-w-a, Som-w-a, Imb-w-a
Kauli ya Kutendana:   Mfano, Pig-an-a, Imb-an-a.
Kauli ya Kutenduka:   Mfano, Tega > Teg-u-a, Fumba > Fumb-u-a
Kauli ya Kutendesha: Mfano, Imb-ish-a, Som-esh-a, Pig-ish-a.

6.      Unyambulishaji unaweza kubadili nafasi ya neno katika muundo wa kishazi au sentensi. Hii ina maana kuwa, neno linaweza kuwa katika nafasi ya nomino katika sentensi, Lakini baada ya neno hilo kufanyiwa unyambulishaji, neno hilo hilo linaweza kubadilika na kuchukua nafasi ya kitenzi katika sentensi.

Mfano.
                        Juma ana utaifa wa Marekani
Ø  Utaifishaji wa Juma ni wa Kimarekani
Katika mfano huu tunaona jinsi ambavyo neno “utaifa”  lilivyoweza kubadilishwa nafasi yake katika sentensi.
Mbali na nduni za Unyambulishaji zilizotolewa na Nchimbi (2008), Lakina pia Unyambulishaji una nduni nyingine kama vile:-
7.      Unyambulishaji pia una sifa ya kuwa na vighaili vingi. Hii ikiwa na maana kuwa , Si kila neno linakubali kuchukua kinyambuzi cha aina ile ile iliyotumika katika maneno mengine.
Mfano.
a)      Tung-a  > Tung-o,
b)      Teg-a  >  Teg-o
c)      Imb-a  > Imb-o
d)     Ib-a  >  Ib-o
Tunaona katika mfano ( c ) na ( d ) Maneno Imba na Iba yameshindwa kuendana na kanuni ya maneno ya mfano ( a ) na ( b ). Hivyo maneno ya mfano ( c ) na ( d ) ni vighaili katika kanuni iliyotumika katika mifano hii.
8.      Vinyambuzi pia siyo zalishi, Hii ikiwa na maana kuwa Vinyambuzi havina tabia ya kujirudia rudia katika neno, na kuwa siyo kila neno linaweza kuambatanishwa na kinyambuzi fulani na kuleta maana.

Mfano
Tenda  > Tend-an a,
Penda  >  Pend-an-a
Kaa > Ka-an -a
Lia > Li-an-a
Katika mifano hii, tunaona jinsi ambavyo kinyambuzi –an- kisivyokuwa zalishi, Kwani kimeshindwa kutumika na kuleta maana katika mfano wa ( iii ) na ( iv ) kama jinsi tulivyoona katika mifano hii.

9.      Kwa kiasi kikubwa sana, Kinyambuzi au vinyambuzi hutokea karibu sana na mzizi wa neno. Ukaribu huu waweza kuwa kabla ya mzizi au baada ya mzizi wa neno.
Mfano.
Piga  >   Pig-an-a
Tulia  >  M-tulivu
Mtoto  >  ki-toto


Kama unahitaji huduma ya kuandikiwa makala katika tovuti yako, au huduma yoyote basi wasiliana nami kupitia:-
SIMU:         +255 755 987 604, +255 789 198 345
E-MAIL:    reubentanzania@gmail.com



HITIMISHO
Dhana ya Unyambulishaji imekuwa ikichanganywa sana na dhana ya Uambishaji (Uambatizi), ijapokuwa matendo haya yote yanahusisha kuongeza viambishi katika mzizi wa neno. Lakini inapaswa tujue kuwa matendo haya yanatofautiana katika uamilifu wake katika isimu ya lugha. Na utofauti huo unatokana na ukweli kuwa Unyambulishaji unahusu kuongeza viambishi katika mzizi wa neno, wakati huo viambishi hivyo vinakuwa na uamilifu wa kuunda neno jipya kutoka katika neno lililofanyiwa unyambulishaji. Kwa upande mwingine, Uambishaji (Uambatizi) wenyewe unahusiana na kuboresha maana ya mzizi wa neno kwa kubeba viambishi vyenye kuchukua dhana ya idadi, nafsi, njeo na dhamira.



MAREJEO
Akmajian, A et al (2001) LINGUISTICS, An Introduction to Language and Communication
                        5thEd.USA:Massachusette Institute of Technology Press.
 BAKIZA (2010) Kamusi ya Kiswahili Fasaha.Nairobi:Oxford University Press,East Africa L.t.d
Kihore,Y.M (2009) Sarufi maumbo ya Kiswahili Sanifu (SAMAKISA) Sekondari na Vyuo.
Dar es Salaam:Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI).
Massamba,D.P.B (2004) Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha.Dar –es-Salaam:Taasisi ya
                        Uchunguzi wa Kiswahili.
Nchimbi,A.S (2008) OFC 008 KISWAHILI.Dar es Salaam:Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.
TUKI (2013:420) Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Toleo la 3.Nairobi:Oxford University Press.










Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MUINGILIANO KATI YA SEMANTIKI NA PRAGMATIKI---ACADEMICIAN BLOG

UTANGULIZI Maana ya Semantiki Richmond (2012   anafafanua maana ya Semantiki kwamba ni tawi la isimu ya lugha linalohusu viyambo ...