MAANA YA FASIHI KWA MUJIBU WA K.W WAMITILA
Wataalamu
wengi wa fasihi wametoa maana ya neon fasihi kulingana na mitazamo yao,ubunifu
wao, falsafa zao na hata uzoefu wao katika uwanja wa fasihi. Makala hii,
imeangazia zaidi katika kuichambua maana ya fasihi iliyotolewa na mwana fasihi Kyallo
Wadi Wamitila katika kitabu chake cha Kamusi
Ya Fasihi; Istilahi na Nadharia, kilichochapishwa mwaka 2003.
Maana ya Fasihi kwa mujibu wa Wamitila (2003)
“Fasihi
ni kazi za kisanaa au zilizotumia lugha kwa usanii na zinazowasilisha suala
fulani pamoja kwa njia inayoathiri, kugusa na huacha athari fulani na uonyesha
ubunilizi na ubunifu fulani na zinazomhusu binadamu”
Fasihi ni kazi ya Kisanaa na yenye kutumia
lugha
Hii
ina maana kuwa, fasihi ni sanaa kama zilivyo sanaa zingine kama vile muziki,
uchoraji, ususi, ufinyanzi n.k, isipokuwa fasihi inatumia lugha ili kufikisha
ujumbe wake, tofauti na matawi mengine ya sanaa.
Fasihi ni kazi inayowasilisha suala fulani pamoja
Fasihi
ni lazima iwe na mada, jambo au tukio mahususi ambalo inawasilisha, na jambo
hilo ni lazima liwasilishwe kwa pamoja. Hii ina maana kuwa, kama jambo au kisa
ni lazima kiwasilishwe chote kwa mtiririko unaofaa na uwe ndani ya kazi moja.
Iwasilishwe kwa njia inayoathiri na kugusa
Lengo
la msanii ni kuufikisha ujumbe katika jamii kama jinsi yeye anavyohitaji ufike
au zaidi yahata ambavyo yeye anahitaji ufike. Ili lengo hilo lifanikiwe, ni
lazima kutumia njia zenye kuweza kumgusa msomaji na kuikonga vyema nafsi na
moyo wake kwa kile msanii alichokiwasilisha. Kwa mfano, msanii anahitaji
kuwasilisha ujumbe juu ya unyanyasaji unaofanywa na baadhi ya viongozi katika nchi,
itambidi msanii atumie sauti za hudhuni zilizojaa manyanyaso na uteswaji
uliokithiri
Fasihi huacha athari
Kutokana
na uhalisia wa fasihi katika jamii nyingi, basi kazi ya fasihi huweza
kusababisha matokeo yoyote kutokea katika jamii. Hii ina maanisha kuwa ujumbe
umefika mahali ulipotakiwa kufika na ndiyo maana ukasababisha matokeo kutokea.
Ubunilizi na ubunifu
Ubunilizi
na ubunifu ni vipengele muhimu sana katika kazi yoyote ile ya fasihi. Fasihi bila
ubunifu ni sawa na makala, kama zilivyo makala zingine. Ni vigumu
kujihakikishia usalama kwa msanii wa fasihi pasipo kutumia ubunifu. Tukumbuke kuwa,
katika jamii kuna makundi ya aina nyingi, hivyo lazima kazi ya fasihi iibue
ukinzani endapo kama unakosoa matabaka yenye nguvu.
Zinazomhusu binadamu
Fasihi
ni zao la jamii, hivyo ni vyema kazi za fasihi zimhusu zaidi binadamu kwani
ndiye mwenye utashi na akiri yenye uwezo wa kufikiri. Hii haina maana kuwa
wahusika wanyama hawahitajiki, lahasha! Kinachozungumziwa hapa ni ujumbe
umuhusu binadamu.
Marejeo
Wamitila K.W (2003) Kamusi
ya Kiswahili; Istilahi naNadharia.Focus
Publication.Nairobi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni