Jumanne, 23 Januari 2018

MJASILIAMALI ANASHAURIWA KUITUMIAJE PESA YAKE?




Tulio wengi huwa tunafikiri kuwa ujasiliamali una watu wake maalumu! Fikra hii ni
potofu kwani mtu yeyote anawezakuwa mjasiliamali endapo kama atatumia muda

wake, akiri yake na nguvu zake kujifunza zaidi juu ya wazo alilonalo au juu ya kazi, taaluma au biashara anayoifanya.
Nyumba na gari za kifahari (Liabilities)

Leo nitashiriki nanyi kuhusu tofauti ya Assets na Liabilities.
Wajasiliamali tuliowengi bado hatujajua kutofautisha assets na Liabilities.

Robert Kiyosaki (1998) alitoa tofauti za maneno haya katika muktadha wa
Kilimo (ni asset)
ujasiliamali.
Kiyosaki alisema kuwa, Assets ni kile kinachoingiza pesa mfukoni mwako, na Liabilities ni kile kinachotoa pesa kutoka mfukoni mwako.
Lakini pia kuna vitu vingine vinawezakuwa asset na pia vinawezakuwa Liability, hii inategemea na matumizi ya
Pikipiki (Ni asset, pia ni Liability)
mnunuzi wa kitu hicho. Kwa mfano, pikipiki ni asset endapo kama utaitumia katika shughuli za bodaboda. Itakuwa ni asset kwasababu itakuwa inakuingizia pesa mfukoni mwako.
Kwa upande mwingine pikipiki inawezakuwa Liability endapo kama utaitumia kama nyenzo ya kupigia misele ili kujitwalia sifa na ujiko mtaani na kuonekana kuwa una pesa.
Watanzania wengi tunakuwa masikini kwasababu tunapenda sana kununua vitu ambavyo siyo assets, lakini katika mawazo yetu huwa tunavisema kuwa ni assets. Kwa
Sofa (Liability)
mfano , utakuta mtu kanunua sofa, kwaajili ya kuweka ndani, lakini wakati huo huo pesa anaipata kwa kufanya kazi ngumu! Yaani kashindwa kuanzisha hata kibiashara

kidogo kikawa kinamuingizia pesa kwa urahisi na badala yake ananunua kitu cha starehe ili tu naye aonekane kuwa anapesa, wakati kiuhalisia hana pesa.
Pengine utakuta mtu kakopa pesa benki, wakati hata hana malengo mahususi na pesa hizo, atakachokifanya ni kununua/kujenge jumba kubwa tena la gharama na gari la kisasa la kutembelea ili aonekane kuwa ni mtu wa kisasa,wakati hana hata biashara yoyote itakayomsaidia kurejesha mkopo huo benki. Matokeo yake benki wanamfirisi na hatimaye anakimbia kujificha ili aepuke aibu! Hayo ni mawazo mgando.
Swali
Kulingana na mtazamo wa Kiyosaki, mtu akinunua “Kiwanja” atakuwa amenunua asset? Au ni Liability!


MUINGILIANO KATI YA SEMANTIKI NA PRAGMATIKI---ACADEMICIAN BLOG

UTANGULIZI Maana ya Semantiki Richmond (2012   anafafanua maana ya Semantiki kwamba ni tawi la isimu ya lugha linalohusu viyambo ...