#1: Taaluma uliyonayo (elimu)
Unaweza
kupata mtaji kwa kuitumia vyema elimu yako! Kuna mambo mawili ya kufanya ili
upate mtaji katika njia hii. Mosi, ni kujiajiri mwenyewe kupitia taaluma
uliyonayo.
Mfano.
1. kama wewe ni
muhandisi wa umeme, basi unaweza ukaanzisha huduma ya kuweka umeme majumbani
(domestic electirical installation). Kupitia hii huduma, unaweza kupata mtaji
na kisha ukafungua duka la vifaa vya umeme. Ni watu wengi waliofanikiwa kupata
mitaji mikubwa kwa kupitia njia hii! Nina mfano wa technician mmoja wa kiwanda
cha saruji kilichopo Songwe- Tanzania (Zephania Lulyeho), yeye alianza kufanya
hivyo kama anajaribu, lakini sasa hivi anamiliki kampuni yake ya JAZA yenye kujishughulisha na masuala ya
kufanya electrical installation.
2. kama wewe ni daktari, basi unaweza kuanzisha kituo
kidogo cha afya! Hata kama kiwe na uwezo wa kutoa huduma ya kwanza, au kutoa
vipimo hata viwili (mf, malaria na taifodi) kinatosha kuanzia. Baada ya kupata
mtaji mzuri, basi utaweza kufungua duka la madawa! Kwani utakuwa tayari una
cheti cha afya, lakini pia utakuwa na kibari cha kukuruhusu kuuza madawa na
vyakula, mfano cheti cha TFDA kwa
upande wa Tanzania.
3. kama wewe ni mwalimu, basi unaweza
ukaanzisha kituo cha masomo kwa muda wa ziada (tution). Kituo hiki utakipatia
majukumu kadha wa kadha kama vile, kozi fupi ya lugha ya Kiingereza, kuwanoa
wanafunzi wa shule za msingi na sekondari na Kuwanoa wale wanaohitaji kurudia
kufanya mitihani ya kidato cha 4 & 6. Haya majukumu ni vigumu kufanywa na
mtu mmoja kwa ufanisi, hivyo unashauriwa kuungana na watu wenye nia na wenye
vigezo vya kufanya kazi hiyo, hata kama iwe nikwakugawana faida.
Lakini, pili (2) ni kuajiriwa katika taasisi, serikali ama mtu
binafsi
#2: Kuomba mtaji kwa wanafamilia, ndugu na
jamaa
Hapa pia kuna mambo ya kuzingatia ili upate
mjati kwa ndugu au jamaako wa karibu
v Onyesha
uwajibikaji
v Msaidie
kazi kwa uaminifu wote
v Tambua
nini anapendelea huyo ndugu yako
v Mpe
mawazo na mbinu za kuiendeleza biashara yake
v Utakapofikia
wakati wa kumwomba mtaji, omba mtaji kidogo
v Baada ya
kupewa mtaji, hakikisha unamshirikisha katika biashara yako. Hii ni pamoja na
kumpatia taarifa juu ya maendeleo ya biashara yako.
#3: Fani/ kipaji
Unaweza
kupata mtaji kupitia kipaji chako! Lakini pia unaweza kukifanya kipaji chako
kama ndiyo ajira yako. Ili kukifanya kipaji kuwa ajira, unashauriwa pia kupata
mawazo mapya kutoka kwa watu, wateja, au washabiki wako, lakini pia soma vitabu
mbali mbali vinavyohusiana na kipaji chako. Mawazo haya ndiyo yatakayokufanya
uwe mbunifu katika fani yako. Unapofanya kazi kupitia kipaji chako, ni vyema
pia ukazingatia uhusiano wa kazi zako na soko la kimataifa. Katika makala
zijazo, tutajadili zaidi juu ya jinsi ya
kutafuta masoko ya kimataifa kwa lazima. Mfano, msusi, mfinyanzi, mchoraji,
mchongaji, mwana muziki, mwandishi nk, hawa wote wanawezaje kupata soko la
kimataifa kwa lazima. Maana, inatakiwa umlazimishe mtu kuwa mteja wako pasipo
yeye kujua kama unamlazimisha kuwa mteja wa bidhaa yako.
#4: Uzoefu katika kufanya kitu fulani
Katika
upande wa masuala ya ajira imekwisha zoeleka kwamba, ili upate ajira basi
unatakiwa uwe na uzoefu wa miaka kadhaa kazini katika kitengo unachoomba kazi.
Ukweli ni kwamba katika mfumo wa uchumi na biashara kwa sasa, mwajiri anaajiri
mtu ambaye anaweza kumrahisishia kazi bila kufundishwa pindi anapokuwa
akitumikia nafasi yake ya kazi ili kuepusha hasara na gharama ambazo hazikuwa
za lazima. Lakini pia, hauwezi kupata uzoefu bila kuanza. Hii nina maana
kwamba, ili upate uzoefu basi fanya kazi hata kwa mfumo wa kujitolea, kwani
kupitia kujitolea utaweza kujuana na watu wengi zaidi na zaidi, na hicho ndicho
mshahara wako.
#5: Ujuzi
Ujuzi nao
ni moja ya mambo muhimu sana katika kukurahisishia kupata mtaji. Hapa zaidi
kinachotiliwa maanani ni ufundi ambao mtu anaupata hata pasipokuwa na elimu
kubwa. Kupitia ujuzi, unaweza kuwa fundi ujenzi wa kisasa, fundi wa vifaa vya
kielekitroniki kama vile, redio,TV,kompyuta,pasi za umeme n.k. watu wengi sana
wana ujuzi mbalimbali, lakini hawana nidhamu ya pesa. Kutokuwa na nidhamu ya pesa,
kunawafanya wawe na maisha yale yale kila mwaka, na hatimaye kuuona ujuzi wao
kama hauwasaidii kabisa katika maisha yao! Jamani TUBADILIKE KATIKA JINSI YA KUFIKIRI MAMBO
#6: Fanya Kitu unachokipenda
Kufanya
kitu unachokipenda ni njia mojawapo muhimu ya kukuongezea mtaji. Kuna watu wana
mitaji midogo na wameshindwa kuiendeleza mitaji hiyo kutokana na kufanya
kitu/biashara wasioipenda. Ni ukweli kuwa, kuna baadhi ya watu hufanya mambo,
kazi au biashara kwa kufuata mihemko ya wazazi, ndugu au rafiki zao, lakini
ndani ya moyo mioyo yao hawaridhiki kabisa. Hali hii itakufanya upunguze
ukaribu na kile unachokifanya, lakini pia unaweza kukosa ubunifu wa kazi/
biashara hiyo kutokana na kutoipenda.
#7: Omba mkopo
Kama una
nia kweli ya kufanya biashara, na una vigezo vya kuzifanya taasisi za kifedha
kukuamini, bai omba mkopo.
ANGALIZO:
1
Usiombe mkopo wa kibiashara, endapo kama
haujaanza biashara, maana fedha ya mkopo siyo fedha ya kuanzisha biashara,
bali ni fedha ya kuendeleza biashara. Nimeeleza mambo mengi sana katika
kitabu change kinachohusu masuala ya mikopo, na siku siyo nyingi
nitakichapisha ili nawe msomaji wangu ujifunze mengi juu ya masuala ya mikopo
kutokana na mengi niliyojifunza kuhusu mikopo.
|
ANGALIZO:
2
Usichukue mkopo endapo kama haujafanya utafiti
wa kutosha juu ya biashara unayoifanya/unayotaka kuifanya.
|
#8: Uuzaji wa rasilimali
Hii nayo
ni njia ya kupata mtaji lakini sikushauri sana kuitumia kwani, siyo rahisi
kuirudisha rasilimali ambayo umekwishaiuza. Kama mtu unayeanza kupambana ili
upate msingi mzuri wa maisha, si vyema kuwa na tabia ya kuuza vitu. Hii ni
kutokana na ukweli kuwa, bei utakayouzia kwa kiasi kikubwa siyo bei rafiki.
Lakini kama ukikwama sana na ukaona njia zingine huwezi kuzitumia basi unaweza
ukauza, lakini uwe na uhakika wa kuirusha rasilimali hiyo unayoiuza.
#9: Kushirikiana na watumishi wa serikali
Kuna
baadhi ya watumishi wa serikali hawana muda wa kuzalisha mishahara yao. Lakini
wapo wengine ambao hata hawana elimu ya fedha. Kutokana na pengo hili, kama
mjasiliamali usiye na mtaji, unatakiwa kupanga biashara na mwelekeo wa hiyo
biashara, na kisha ukamshirikisha mtumishi ambaye anaonekana kutokuwa na
uwekezaji wowote wa fedha yake.
ANGALIZO
Mjasiriamali unatakiwa kuwa na tarifa za uhakika
juu ya biashara unayoipendekeza, na hizi taarifa unaweza kuzipata kupitia
kufanya utafiti wa kutosha juu ya biashara hiyo. Mfano, je ni biashara ya
msimu?, faida yake, hasara zake zinasababishwaje? Jinsi ya kuzuia hasara,
wateja wa biashara hiyo ni watu gani? N.k. kwa kufanya hivyo, utaweza kufanya
biashara ambayo itakunufaisha wewe pamoja na Yule aliyewekeza fedha yake
katika biashara hiyo.
|
#10: Ufugaji
Kama una
mtaji wa eneo, basi fanya ufugaji wa mifugo ili upate mtaji unaouhitaji ndani
ya kipindi kifupi. Kuna mifugo wengi ambao unaweza ukawafuga, mfano, kuku wa
kienyeji, bata wa kawaida, bata maji, bata mzinga, sungura, kanga, kwale,
nguruwe n.k. hawa wote wana uwezo wa kukupatia mtaji kwa muda mfupi. Cha muhimu
ni kufugakibiashara, na kutafuta masoko yenye tija.
Katika
biashara, mambo ya muhimu unayotakiwa kuwanayo ni UKWELI na UAMINIFU!
Utapata wateja waminifu na utapata mtaji hata bila kuomwomba mtu, ila yeye
atakuletea fedha yake uifanyie uzalishaji
Nakushukuru kwa
kufuatilia makala zangu katika blog yangu na katika kurasa zangu za mitandao
ya kijamii. Usikose kufuatilia makala zangu zingine, ni rahisi sana, ingia
kwenye blog yangu kisha bofya kitufe follow
by e-mail. Mpaka
hapo utakuwa umefanikiwa kupata makala zangu mpya.
|